Your Cart

About Me

Naitwa Geofrey Dismas ni mtunzi na mwandishi wa hadithi na simulizi. Nilianzisha HADITHI ZETU kwa lengo la kuwafikia wapenzi wa hadithi na simulizi kidigitali. Kutunga na kuandika hadithi ni burudani yangu hivyo kila wakati najitahidi kadiri niwezavyo kutunga hadithi na simulizi nzuri kwa ajili ya kila mtu.

KUHUSU HADITHI ZETU

HADITHI ZETU ni wazo ambalo lilikuwepo tangu mwaka 2010. Wazo hili lilikuwa kuanzisha platform ambayo itakusanya kila kazi ya fasihi na kuiweka sehemu moja kwa ajili ya kuwapa wapenzio wa kazi ya fasihi burudani. Lakini Mwaka 2015 wazo likaboreshwa na kutengenezwa wazo la kujumuisha kila kitu kinachohusu burudani, kuanzia VITABU, MAKALA, VIDEO, HABARI ZA BURUDANI nk na hapo ndipo ilipofikia mwaka 2020 ambapo wazo likatoka kuwa wazo na kuwa kitu halisi. HADITHI ZETU tupo na matawi yafuatayo; Hadithi Zetu Blog kwa ajili ya kuhabarisha wapenzi wa burudani mbambo ya burudani na hasa kazi ya FASIHI SIMULIZI na ANDISHI , Hadithi Zetu Store ambapo hapa bidhaa za kila aina zinauzwa hapa ikiwemo kazi za FASIHI.


KARIBU TUFURAHIE BURUDANI KWA PAMOJA.